Duniani kuna mambo ya ajabu sana,
Wenye muda wengi wao hawana pesa,
Na wenye pesa nao hawana muda kabisa.
Masikini kijiweni wanajadili maisha ya watu,
Kuhusu mpira, mapenzi na mabishano yasiyo na mwisho,
Muda unapotea, umaskini unazidi kutesa.
Bila hekima yako Mungu tutafika tumechoka,
Tusaidie Mungu wetu, sisi waja wako.
Utupe macho ya kuona, na akili ya kuvuka,
Bila hekima yako Mungu tutafika tumechoka.
Tusaidie Mungu wetu, sisi waja wako.
Tusaidie Baba...
Sisi waja wako...
Hekima yako pekee.