[male vocals] TAMALA
Tamala
wanizuzuwa,
na
hilo
pendo
ambalo
Mwenzio
ninapagawa,
na
huba
nilipatalo
Na
hasa
ninauguwa,
nisijijue
kwa
hilo
Si
tende
siyo
haluwa,
utamu
niuhisio.
Ona
navyojimwagia,
dabwa
machozi
shavuni
Sikai
nikatulia,
hemuhemu
ni
ndiani
Kaumu
wanidhania,
majununi
akilini
Ni
huba
lanizuzua,
hilo
hawajabaini.
Naradidi
kwa
karara,
nudhumu
nakutungiya
Ikufike
tajamala,
heri
nakusabiliya
Kwako
isiwe
hasara,
mahaba
kinigawiya
Jitume
kugangamala,
hatamu
kujishindiya.
Kwako
weye
sifukuti,
penzi
nimeshaliridhi
Kwa
huba
najidhatiti,
nisitoke
kwenye
jozi
Wache
waunde
kamati,
ndizo
za
kwao
walozi
Kwako
mefika
tamati,
bendera
naikabidhi.