Yeah... Sir Nixy...turn the lights down low...
Kaa karibu nami kwenye mawazo...
Sikiliza moyo wangu unavyodunda kwa ajili yako...
Mmh, yeah...
Najua usiku umefika mpenzi,
Nawe unakaribia kupumzika, kitandani umejisogeza,
Macho yanaanza mzigo wa usingizi, uzuri wako unanifanya nitelemke,
Lakini kabla niseme usiku mwema, kuna jambo naliwaza,
Naomba uniambie kitu kutoka ndani ya moyo wako,
Kitu kimoja tu, ambacho kitaleta furaha kwa roho yangu,
Niambie mpenzi, nishibishe nafsi kabla sijaingia gizani...
Goodnight sweetheart... (Malaika wangu)
Usiku mwema moyo wangu... (Ufunguo wa maisha yangu)
Usiku mwema mpenzi wa moyo wangu... (Kipenzi changu)
Lala salama mwandani wangu...
(Usiwaze kitu, nipo hapa kwa ajili yako)
Funga macho yako taratibu, acha miujiza ichukue nafasi,
Niko hapa kukulinda kwenye ulimwengu wa ndoto,
Usiwe na shaka, penzi langu ni blanketi lako la joto,
Linalokukumbatia kwa upole na kukupa faraja,
Tabasamu lako liwe nuru ya chumba chako usiku wa leo,
Usingizi ukuchukue kwa amani, bila hofu, bila mawazo...
Goodnight sweetheart...(malaika wangu)
Usiku mwema moyo wangu...(Ufunguo wa maisha yangu)
Usiku mwema mpenzi wa moyo wangu...(Kipenzi changu)
Lala salama mwandani wangu...(Usiwaze kitu,nipo hapa kwa ajili yako)
Lala sasa, malkia wangu...
Acha malaika wakulinde...
Moyo wangu unadunda kwa ajili yako tu...
Kesho ni siku mpya ya kukupenda zaidi...
Goodnight, my love...
Sir Nixy!