Msiniachie Vituoni”*
_Ujumbe kwa Madereva wa Daladala_
***_
Dereva, dereva, sikiliza kilio changu mtoto wa YOMBO VITUKA SEKONDARI
Mimi ni mwanafunzi, ndoto yangu iko mbele.
Usipite haraka, usiniachie vituoni,
Kila dakika kwangu ni hatua ya maisha.
*[Betri ya Kwanza]*
Ninasimama na kitabu mkononi,
Ngoja uniokoe, unipe nafasi.
Ukiniache leo, kesho ninaweza kukosa somo,
Na somo hilo linaweza kuwa ufunguo wa maisha yangu.
*[Betri ya Pili]*
Wewe ni baba yangu njiani, mlinzi wa safari,
Mshiriki wa ndoto yangu bila kujua.
Ukinipeleka salama, unajenga taifa,
Leo mwanafunzi, kesho daktari atakayekuponya.
_**_
Msiniachie vituoni, msinizime matumaini,
Nibebe kwa upendo, nibebe kwa heshima.
Yombo Vituka, Temeke, Tanzania inategemea,
Dereva, uwe sehemu ya mafanikio yangu![Mshororo]
_***
Dereva, dereva, moyo wako uwe mpole,
Kila mwanafunzi ni taifa linalosimama.
Tushikane mikono, safari iwe salama,
Pamoja tutafika, pamoja tutashinda!